WANANCHI WAHIMIZWA KUPANDA MITI KUTUNZA MAZINGIRA

Na Mwandishi wetu.
Wananchi
wa Kata ya Isakalilo wameshauriwa kuwa na utamaduni wa upandaji wa miti ili
kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi
Pamoja na urejeshwaji wa uoto wa asili uliopotea katika mazingira
yanayowazunguka.
Hayo
yamesemwa na Daniel Kalinga ambaye ni Mkurugenzi wa Shule ya Awali na Msingi
KALDAN, iliyoko katika kata ya Isikalilo mtaa wa Kitasengwa ndani ya manispaa
ya Iringa alipokuwa anazungumza na wananchi wanaoishi karibu na shule mara
baada ya kukabidhi miti ya matunda ya Mparachichi kwa kila mmoja.
Kalinga
amesema kuwa wananchi hawana budi kuendelea na utunzaji wa misitu Pamoja na
upandaji wa miti na kwa mazingira ya Kitasengwa yamezungukwa na miti hivyo
hatuna budi kuanza kupanda miti ya matunda licha ya kusaidia utunzaji wa
mazingira ila ni chanzo kizuri cha mapato kwa mwananchi.
Aidha
amesema kuwa upandaji wa miti wananchi
wanaweza kupanda miti yenye manufaa ikiwemo ya matunda kama vile miembe,,mipapai , mpera na miti
mingine ya matunda ambayo inaweza kuwa sehemu ya kilimo na wakati mwingine
ikitunza mazingira .
Akizungumzia
mikakati ya shule hiyo mazingira eneo la Kitasengwa katika utunzaji wa
mazingira na upandaji wa miti amesema kuwa wanaendelea na uboreshaji na utaratibu wa kuwa na klabu za wanafunzi
mashuleni ili baadae wawe msaada mkubwa
wa kuelimisha jamii juu ya utunzaji wa
Mazingira.
Kwa
upande wao baadhi ya wananchi afisa walimshukuru Mkurugenzi Daniel Kalinga kwa
kuonyesha moyo wa Kutunza mazingira na kuwapatia miti ya Mparachichi kwani licha
ya kuwa faida kwao ila itasaidia kutunza mazingira.
Mmoja
ya wananchi walipokea miti hiyo Daniela Mtanda ameelezea umuhimu wa uwepo wa
miti na misitu katika Maisha ya binadamu kuwa ni Pamoja na upatikanaji wa dawa
,vyakula Pamoja na kusaidia kuzuia mmonyoko wa udongo.
No comments