Breaking News

WAZAZI NA WALEZI WAPEWA SOMO, MALEZI BORA YA WATOTO


N Fatma Rajab.
 Wzazi na waleziwa wametakiwa kuwalea watoto wao katika madili yaliokuwa Bora ili kuepukana na changamoto mbali mbali ambazo zinaweza kujitkeza kwa watoto   hususani katika kipndi hichi cha kuelekea uchaguzi mkuu wa zaznibar.‎

‎Hayo yameelezwa na   Mkurugenzi wa Idara  ya maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Siti Abas Ali katika mafunzo ya kutoa elimu ya malezi kwa waratibu kutoka shehia zote za Unguja pamoja na wazazi na walezi kuhusiana  malezi hafla iliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa skuli ya sekondri   Tumekuja. 

Amesema lengo la kuanzishwa kwa mafunzo Hayo ni  kuweza kusimamia  malezi na tamaduni za kizanzibari, ''ni lazima watoto walindwe wasimamiwe  wapatiwe elimu iliyobora ili kuweza kupata viongozi waliokuwa bora wa baadae kwani vijana ndio Taifa la kesho''  ameeleza Mkurugenzi Siti

Aidha amewakumbusha  wazazi na walezi kuzungumza na vijana wao wajiepushe na kukaa na watu  wanaofanya  uvunjifu wa  amani hususani katika kipindi hichi cha uchaguzi, kwani amani ikivunjika waathirika wakubwa ni wanawake na watoto.sambamba na hilo amewataka wazazi na walezi kutowahusisha watoto na vyama vya kisiasa ili kuepusha changamoto mbali mbali  zinaweza kujitokeza kwa jamii.

‎‎Nae meneja wa mradi wa mafunzo ya malezi ya kinababa na kinamama katika Jumuiya ya Vijana elimu Maendeleo ya Mazingira Zanzibar ( ZAYADESA ) Aisha Ali  Amani Karume  Amesema kuwa lengo la mafunzo Hayo  ni wawezesha wazazi namna ya kuwalea watoto katika mazingira bora na kuwakinga  kuingia katika makundi hatarishi. Pamoja na  kuelewa changamoto mbali mbali ambazo wanakabiliana nazo.

‎Kwa upande wao wazazi na walezi waliopatiwa mafunzo hayo wamesema mafunzo Hayo yamewasaidia kujua jinsia Gani wanaweza kuwalea watoto wao wa kike na wakiume kirafiki ili kuweza kuwafikishia matatizo yao na changamoto na kujua ni jinsi Gani wanaweza kuzitatua changamoto hizo. 

‎ Mafunzo Hayo yameandaliwa na taasisis ya ZAYADESA kwa kushirikian na mama shadiya karume ya kutoka elimu kwa wazazi wa kike na wakiume na mafunzo Hayo yamechukuwa takribani wiki kumi kwa kuwakutanisha wazazi na walezi katika wilaya zote za Unguja



No comments