Breaking News

WAKULIMA WANAWAKE VIONGOZI TUMIENI VYOMBO VYA HABARI MTAKOMBOKA


Na Thuwaiba Habibu, Zanzibar 

Meneja  Miradi kutoka chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA-ZNZ Nairat Abdulla amewahimiza wanawake  viongozi  kutumia vyombo  vya habari kueleza mafanikio na changamoto zinazowakabili katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya Nchi.

Ameyasema  hayo wakati wa mafunzo ya wanawake viongozi juu ya kukabiliana na mabadiliko ya ya tabia ya nchi yaliofanyika katika ofisi za TAMWA  Tunguu  Zanzibar yenye lengo la kurejesha hali halisi ya visiwa hivyo.

Amesema wanawake  viongozi wanatakiwa watumie vyombo vya habari ili waweze kuonesha mafanikio na changamoto wanazopitia katika shughuli za kimaendeleo wanazo zifanya hasa hizi za kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi ili kupata ufumbuzi wa changamoto  hizo.

Aidha aliwasihi kuwa mabalozi kwa jamii zao kuhakikisha wanakabiliana na changamoto zote za mabadiliko ya hali ya nchi ikiwemo kupanda miti,kutoharibu mazingira kwa kuchimba michanga na kuzuiya wasiharibu uoto wa asili ili kudumisha mandhari mzuri ya nchi .

Katibu wa kikundi cha Huruma hailei Mwana na Mjumbe wa sheha kutoka sheria ya bungi Salma Shija Masanja  amesema  kuwa baada ya kuja kwa mradi wa zan adapt katika mkoa wao wa kusini kumewasaidia wanawake wengi kujuwa mbinu  mzuri za kuhifadhi mazingira kutokana  na mabadiliko ya tabia ya nchi ambayo yapo. 

Nae  Mkulima kiongozi kutoka Unguja ukuu kae Pwani Zakia Mansabu amesema wana mafanikio makubwa baada ya kuja kwa mradi huu wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi  kwani wameweza kurejesha uoto  wa asili  na kuhifadhi mazingira kutokana elimu ya kutunza mikoko na kupatiwa miti13,887 ambayo tayari imeshapanda. 

Kwa sasa tumepiga hatua katika suala zima la kukaliana na mabadiliko ya tabia ya nchi kwani kuna wasimamizi wa kuangalia mazingira yasihariwe na jamii inaelewa umuhimu wa jambo hili.

Pia walishukuru  kupatiwa mafunzo hayo kwani yamewasaidia katika kutunza mazingira na wameahidi watahakikisha wataongeza kupanda miti na kutumia elimu hiyo kuelimisha wengine.



No comments