CEJG YATOA ELIMU YA SHERIA NA UTAWALA BORA KWA WILAYA YA KASKAZINI B ILI WANANCHI WAJUE HAKI NA WAJIBU WAO.
NA SITI ALI.
Kwa miaka mingi,jamii nyingi zimekuwa zikikabiliwa na changamoto
ya uwelewa mdogo wa sharia,haki za binaadamu na utawala bora.Hali hiyo
imechangia kuendelea kwa migogoro,vitendo vya ukatil,unyanyasaji na
ubaguzi,huku wananchi wengi wakikosa uelewa wa namna ya kulinda haki zao na
kupata msaada wa kishehia.
Kutokana na changamoto hizo,Idara ya Maendeleo ya Kanisa
Katoliki Kanda ya Zanzibar kupitia Mradi wa Uwezeshaji wa Jamii kwa ajili ya
Haki za Binaadamu na Utawala Bora Awamu ya Tano (CEJG Phase V)unaofadhiliwa na
Misereor,imeendelea kutoa elimu ya msaada wa kisheria,haki za binaadamu na
utawala bora katika shehiya ya Mahonda,Mkataleni Kitope,Donge Majenzi na Bumbwini
Misufini,Wilaya ya Kaskazini B Unguja.
Mbali na kutoa elimu kwa wananchi,mradi huo unashirikiana na
Wasaidizi wa Sheria Kaskazini B pamoja na kamati ya uwajibikaji na utawala bora
ili kuimarisha ushiriki wa jamii katika kulinda haki za wananchi,kuhamasisha
uwajibikaji na kurahisisha upatikanaji wa haki kwa wanawake,vijana,watoto na
watu wenye ulemavu.
Kupitia mafunzo hayo,wananchi wameendelea kujifunza kuhusu
haki zao za msingi,wajibu wao kama raia,umuhimu wa kushiriki kaika maamuzi ya
maendeleo,pamoja na namna ya kuripoti vitendo vya ukatili,unyanyasajina
ukiukwaji wa haki kwa kutumia mifumo iliyopo.
Afisa ufuatiliaji na Tathmini wa mradi huo Msafiri Thomas
Mombo amesema uamuzi wa kuanzisha mradi ulitokana na matokeo ya tathmini
iliyoonesha kuwa bado kuna uelewa mdogo wa sheria na haki za binaadamu katika
baadhi ya jamii za Zanzibar.
Amesema wananchi wengi hawafahamu kikamilifu haki zao wala
namna ya kuzitetea,jambo linalochangia kuendelea kwa migogoro na ukiukwaji wa haki
za binaadamu kwa mujibu wake,kuwajengea wananchi uwezo wa kupata elimu ni hatua
muhimu katika kujenga jamii inayozingatia usawa, Amani na utawala bora.
“Wanawake wakipewa elimu
sahihi katika shehiya wanakuwa rahisi kuelewa masuala ya haki,wajibu usawa na
Amani katika maisha yao ya kila siku.”amesema Mombo.
Ameongeza kuwa utekelezwaji wa mradi utaendelea kutanuliwa
ili wananchi wengi Zaidi waweze kunufaika,huku kamati pamoja na wasaidizi wa
sheria wataendelea kuwa ni daraja muhimu la kuelimisha jamii kupitia mikutano,
mijadala,na shughuli mbalimbali za kijamii.
Kwa upande wake Mwanasheria wa Mradi huo Peter Marwa,amesema
kuanzishwa kwa mradi huo ni uwekezaji muhimu katika kujenga jamii inayo tambua
haki na wajibu wake na kuimarisha upatikanaji wa haki pamoja na misingi ya
utawala bora.
Ameeleza kuwa wananchi wataendelea kupewa elimu ya misingi ikiwemo
haki ya elimu,haki ya kuishi bila ya ukatili, haki ya kushiriki katika maamuzi
yanayowahusu aidha ameongeza kuwa elimu hiyo itawasaidia wananchi kuwa mabalozi
wa haki katika familia na jamii zao.
Aidha amesema kuwa Zanzibar bado inakabiliwa na changamoto ya
ukatili na udhalilishaji wa kijinsia na ukiukwaji wa haki mbalimbali kutokana
na hiyo kuna umuhimu wa kuwajengea uwezo wananchi wa kujilinda,kutoa taarifa
wanapoona vitendo vya ukatili na kutafuta msaada wa kisheria kupitia taasisi
husika.
Viongozi wa shehiya wameeleza kuwamafunzo hayo yameongeza
uelewa wa wananchi kuhusu sharia na kupunguza mogogoro inayotokana na
kutofahamu haki na wajibu wao.Sheha wa shehiya ya Mahonda Ali Issa Kinole,amesema
elimu hiyo itawasaidia wananchi kuishi kwa kuzingatia sheria,maadili na
kuheshimiana.
Naye Mkurugenzi wa Taasisi ya Wasaidizi wa Sheria Wilaya ya Kaskazini
B Shaaban Sariboko Makarani,amesema kuwa Utawala Bora unahitaji Sheria
kutekelezwa kwa usawa bila ubaguzi,huku makundi yote ya jamii yakipewa fursa
sawa za kushiriki katika maendeleo.
“Utawala bora lazima za haki zitekelezwe bila ubaguzi wowote.
Hakuna mtu au taasisi iliyo juu ya sheria, kuanzia viongozi wakuu hadi
mwananchi wa kawaida. Hii inajumuisha pia ulinzi kamili wa haki za binadamu”ameeleza
Sariboko.
Kwa upande wa Shehe na Imamu katika Shehiya ya Mahonda Shehe
Salum Gharib Salum amesema kuwa elimu hiyo itawasaidia wananchi kuwaelimisha
wenzao ili kujenga jamii inayoheshimu hakiza binaadamuna kupinga vitendo vya
ukatili na unyanyasaji.
“Wanajamii waliopatiwa elimu hiyo watajitahidi kuwafundisha
wenzao ili elimu hiyo izidi kuenea Zaidi katika shehia pamoja na jamii
zinazowazunguka kwa manufaa ya nchi na taifa kwa ujumla.”ameeleza Shehe
Mnufaika wa mafunzo hayo kutoka Donge Majenzi Rehema Haji
Seif amesema mafunzo hayo yamewawezesha kuelewa haki zao na kuwapa ujasiri wa
kutumia mifumo ya kisheria kutafuta haki wanapokumbana na changamoto.
“Tunashukuru kanisa katoliki kanda ya Zanzibar kupitia Mradi
wa Uwezeshaji wa Haki za Binadamu na Utawala Bora kwa kutupatia mafunzo haya
kwani tumepata uwelewa wa kutosha juu ya masuala ya haki na sheria na kuziomba
shehia kuwa sehemu salama kwa wananchi kupeleka malalamiko yetu bila ya hofu na
vitisho”ameeleza Rehema.
Kwa ujumla utekekelezwaji wa mradi huo wa uwezeshaji wa jamii
kwa ajili ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora Awamu ya Tano unaonesha dhamira
ya Idara ya Maendeleo ya Kanisa Katoliki Kanda ya Zanzibar ya kujenga jamii inayotambua
haki na wajibu wake,inayoshiriki kikamilifu katika utawala bora na inayoheshimu
misingi ya haki za binaadamu.Kupitia elimu ya msaada wa kisheria,uhamasishaji
jamii na ushirikiano na viongozi wa serikali,viongozi wa dini na wadau mbali
mbali wa maendeleo,mradi unaendelea kuweka msingi wa jamii yenye
Amani,usawa,uwajibikaji na maendeleo endelevu Zanzibar.
Mwisho.

.jpeg)

No comments