Breaking News

MIAKA 62 YA MAPINDUZI ZANZIBAR YAIPAISHA SEKTA YA ELIMU




NA SITI ALI.

Mapinduzi ya Januari ya mwaka1964 ni tukio muhimu katika historia ya Zanzibar ambapo ni mwanzo wa safari ya maendeleo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Kwa maana hiyo, maadhimisho ya sherehe za Mapinduzi ni kutathmini mafanikio na malengo ya Mapinduzi kwa dhamira ya waasisi ambayo ni kujikomboa na kuleta maendeleo kwa wananchi wote.

Mwaka huu wa 2026, nchi ya inatimiza miaka 62 ya Mapinduzi ikiwa na kauli mbiu isemayo: Amani na Umoja, Ndio Msingi wa Maendeleo Yetu, “Mapinduzi Daima”. Kauli mbiu hii inayakisi mafanikio makubwa ambayo yamepatikana katika nchi tokea Mapinduzi Matukufu ya mwaka 1964, yametokana na msingi wa amani na umoja na jitihada za viongozi wa Awamu zote za uongozi hapa Zanzibar na ushirikiano mkubwa wa wananchi.

Serikali ya Awamu ya Nane ilipoingia madarakani mwaka 2020, iliahidi kudumisha mafanikio ya Awamu zilizotangulia za uongozi na kuyatafsiri malengo ya Mapinduzi kwa vitendo kwa kuleta mageuzi makubwa ya kiuchumi, kisiasa na kijamii na kuimarisha misingi ya amani, umoja na mshikamano kwa manufaa ya wananchi wote.
Maadhimisho ya miaka 62 ya Mapinduzi ikiwa ni mwanzo wa kipindi cha pili cha uongozi wa Serikali ya Awamu ya Nane. Ambapo imeelezea vipaumbele na mwelekeo wa mipango ya Serikali kwa kipindi cha pili.Ambapo kwa muhtasari mafanikio na mwelekeo wa mipango ya Serikali kwa kipindi cha mwaka mmoja ujao.


Akilihutubia Taifa katika Maadhimisho ya miaka 62 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar Raisi wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Daktari Hussein Ali Hassan Mwinyi amesema kuwa serikali ya awamu ya nane imejipanga kuimarisha huduma kwa jamii ikiwemo elimu,ambayo ni miongoni mwa malengo ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar. Serikali imeifanya sekta ya elimu kuwa kipaumbele kwa kuzingatia umuhimu wake katika kuandaa nguvu kazi na kuchochea maendeleo ya nchi.

“Mageuzi makubwa yaliyofanywa na Serikali katika sekta ya elimu ya ujenzi wa Skuli za kisasa zikiwemo za ghorofa 35, upatikanaji wa vifaa vya kujifunzia, na kufundishia, vifaa vya maabara za masomo ya sayansi na teknolojia, ajira mpya za walimu na kuwapatia mafunzo, kumechangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha mazingira ya Skuli na kuongeza kiwango cha ufaulu wa wanafunzi katika mitihani ya Taifa.

Kwa lengo la kuendelea kuimarisha sekta ya elimu, Serikali itaendeleza ujenzi wa miundombinu ya elimu kwa kujenga Skuli za kisasa za ghorofa ili kukabiliana na changamoto ya msongamano wa wanafunzi madarasani”ameeleza Mheshimiwa Raisi Daktari Mwinyi.
Aidha amesema kuwa Katika kwenda sambamba na mageuzi ya elimu wa mtaala mpya, jumla ya Skuli 70 zitaunganishwa na mkonga wa mawasiliano, kompyuta 2,000 za mezani zitatolewa kwa ajili ya maabara za Skuli, laptop 4,000 zitatolewa kwa ajili ya wanafunzi na kuanzisha smart classrooms 25 ili kuimarisha kujifunza na kufundisha kwa kutumia TEHAMA.
Pamoja na kusema kwamba Kwa mwaka 2025/2026, Serikali imepanga kuajiri walimu wapya 1,500 ili kupunguza tatizo la uhaba wa walimu hasa wa masomo ya sayansi. Aidha, tutaendeleza ujenzi wa dakhalia za wanafunzi na utoaji wa mafunzo ya walimu ili kuwaongezea maarifa pamoja na kuimarisha maslahi yao.


Vile vile, tunaongeza bajeti ya mikopo ya elimu ya juu ili kuwezesha wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu kutapa huduma hiyo kwa uhakika
“Jumla ya Skuli 70 zitaunganishwa na mkonga wa mawasiliano, kompyuta 2,000 za mezani zitatolewa kwa ajili ya maabara za Skuli, laptop 4,000 zitatolewa kwa ajili ya wanafunzi na kuanzisha smart classrooms 25 ili kuimarisha kujifunza na kufundisha kwa kutumia TEHAMA.

Kwa mwaka 2025/2026, Serikali imepanga kuajiri walimu wapya 1,500 ili kupunguza tatizo la uhaba wa walimu hasa wa masomo ya sayansi. Aidha, tutaendeleza ujenzi wa dakhalia za wanafunzi na utoaji wa mafunzo ya walimu ili kuwaongezea maarifa pamoja na kuimarisha maslahi yao.
Tunaongeza bajeti ya mikopo ya elimu ya juu ili kuwezesha wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu kutapa huduma hiyo kwa uhakika”amesema Daktari Mwinyi.

 Akizungumza na waandishi wa habari katika kikao cha tathmini miaka 62 ya mapinduzi ya Zanzibar huko katika ukumbi waSheikh Idrisa Abduli wakili Kikwajuni Makamo wa Pili wa Raisi wa Zanzibar Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla amefafanuwa kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imefanikiwa kufunguwa miradi 64, ambapo iliyowekwa mawe ya msingi ni 46 kwa Unguja na 68 Pemba miradi 42 hivyo hatuwa hizo zinakuja kwa makusudi kuboresha maeneo yete sekta ya elimu
“Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imefanikiwa kufunguwa miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo ya elimu, miradi 64, imefunguliwa ambapo iliyowekwa mawe ya msingi ni 46 kwa Unguja na 68 Pemba miradi 42 hivyo hatuwa hizo zinakuja kwa makusudi kuboresha maeneo yete sekta ya elimu ambapo ni maendeleo makubwa ukilinganisha na miaka ya nyuma”amesema Mheshimiwa Hemed.

Bwana Khamis Juma Kombo mkaazi wa Vikokotoni ameelezea mapinduzi ya mwaka 1964 kupitia sekta ya elimu ambapo imeleta mabadiliko makubwa na amesema kuwa  kabla ya mapinduzi kwa upande wao ilikuwa suala la elimu ni ndoto walioishi nao na haikuwa rahisi kuitimiza kwa kuwa ilikuwa ni ya watu maalumu ingwawa walikuwa na hamu ya kutimiza malengo yao kupitia sekta hiyo
Hivyo walilazimika kufanya kazi zilizokuwa za nguvu kwani elimu wakipata watu wenye hadhi na muonekano maalumu ambao ni wenye uwezo wa kifedha na kiutawala hukuwao wakifanya kazi za kitwana ikiwemo ulinzi na ukulima.
“Kabla ya mapinduzi kwa upande wetu ilikuwa suala la elimu ni ndoto tulioishi na haikuwa rahisi kuitimiza kwa kuwa ilikuwa ni ya watu maalumu ingwawa tulikuwa na hamu ya kutimiza malengo yetu kupitia sekta hiyo

Hivyo tulilazimika kufanya kazi zilizokuwa za nguvu kwani elimu wakipata watu wenye hadhi na muonekano maalumu ambao ni wenye uwezo wa kifedha na kiutawala hukuwao wakifanya kazi za kitwana ikiwemo ulinzi na ukulima”amesema Bwana Khamis.
Mwalimu mstaafu wa skuli ya sekondari ya Tumekuja amesema kuwa miaka 62 ya mapinduzi ya Zanzibar imeleta mabadiliko makubwa katika sekta ya elimu ambapo kuna ongezeko kubwa la maskuli yakiwemo ya horofa na kupelekea kuongezeka kwa ufaulu kwa wanafunzi na kupelekea kupata maendeleo makubwa.


“Miaka 62 ya mapinduzi ya Zanzibar imeleta mabadiliko makubwa katika sekta ya elimu ambapo kuna ongezeko kubwa la maskuli yakiwemo ya horofa na kupelekea kuongezeka kwa ufaulu kwa wanafunzi na kupelekea kupata maendeleo makubwa”amesema Mwalim

Mwanafunzi wa Kidatu cha nne katika skuli ya sekondari ndugu Khadija Juma amesema kuwa wanaishukuru serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kwa kuwapatia elimu bora yenye manufaa bila ya ubaguzi ambapo ndio lengo halisi la mapinduzi ya mwaka 1964 la elimu bora kwa wote.
“Tunaishukuru serikali ya awamu ya nane chini ya uongozi wa Daktari Hussein Mwinyi kwa kutufanikisha kusoma bila ya ubaguzi ambao hata sisi watoto wa wakulima na wakwezi tunasoma bila ya kikwazo chochote na kufanikisha kupata elimu bora bila ya ubaguziambapo ni tofauti na kabla ya mapinduzi ya mwaka 1964” amesema mwanafunzi huyo.

Sekta ya elimu ndio chachu ya maendeleo katika nchi, hivyo basi ni vyema kwa wananchi kuyashukuru na kuyalinda mapinduzi ya 1964 ya Zanzibar ili yaweze kudumu na kuhakikisha kila mtoto wa mkwezi na mkulima anasoma sawa na mtoto wa tajiri bila yaubaguzi wa aina yoyote kwani miaka 62 ya mapinduzi imeleta taswira nzuri katika sekta ya elimu.
Mafanikio makubwa ambayo nchi inajivunia ni kuendelea kuwepo kwa amani nchini. Hii ni nguzo muhimu katika kufanikisha utekelezaji wa mipango yote ya maendeleo na ustawi wa Taifa. Ni vyema kusisitiza umuhimu wa kuitunza amani na kuendelea kuwa wamoja na wenye mshikamano. Kwa kufanya hivyo, nchi itazidi kupiga hatua kubwa zaidi za maendeleo tunayoyatarajia kwa faida watu wote.Kwani bila ya Amani nchi haiwezi kupata maendeleo.


No comments