ZIJUE TIMU ZILIZOYAAGA MASHINDANO YA KLABU BINGWA ULAYA.

Msimu wa Klabu Bingwa Ulaya (Champions League) wa mwaka 2025-26 umeanza kuchanja mbuga na kufikia katika hatua ya kuwatofautisha timu ndogo na timu vigogo.
Ijapokuwa kila timu imesalia na mechi za raundi moja kabla ya hatua ya muondowano wa raundi ya 16, tayari kuna timu ambazo zimeyaaga mashindano hayo ya kifahari zaidi barani Ulaya.
Mfumo huu mpya wa klabu bingwa ulaya ulioanzishwa msimu uliopita, unajumuisha jumla ya timu 36, timu 24 zitafuzu kuingia hatua ya mchujo wa muondowano yaani KO. Kutoka hapo timu 16 zitaingia raundi ya 16 nazo timu 12 zitafungashwa virago na kujaribu tena mwakani.
Hebu tuanze na timu ambazo zishatolewa katika ngarambe hizi, ya kwanza ni Villarreal ya Uhispania.
Timu hiii inayoshikilia nafasi ya tatu katika ligi kuu ya soka nchini Uhispania imewashangaza mashabiki wengi jana usiku baada ya kurindimwa na Ajax ya Uholanzi kwa kichapo cha mabao 2-1 tena wakiwa uwanja wa nyumbani Estadio de la Cerámica.
Timu ya pili ilitolewa kwenye michuano hii ni Kairat Almaty kutoka Kazahkstan.Walitolewa baada ya kipigo cha mabao 4-1 dhidi ya Club Brugge ya Ubelgiji.
Hata hivyo timu hii imejifunza mengi kwani ndio mara ya kwanza katika historia kushiriki katika michuano hii.
Kwa mantiki hiyo,baada ya mechi za Jumanne usiku mabingwa mara 15 wa klabu bingwa Real Madrid ya Uhisania,Tottenham, Sporting CP, Inter Milan, Atletico Madrid wote wamejikatia tiketi ya kufuzu hatua ya muondowano wakiungana na Arsenal iliyofuzu hata kabla ya mechi ya jana dhidi ya Inter Milan.
No comments