Breaking News

WAZIRI SHAABAN ATOA WITO WA MASHIRIKIANO ILI KUKUZA AJIRA ZA VIJANA ZANZIBAR

 


Na Fatma Rajab    24/11/2025.

Waziri wa Vijana Ajira  na Uwezeshaji Mhe. Shaaban  Ali Othman  amewataka watendaji wa Wizara hiyo Kuendeleza mashirikiano pamoja na  kubadilika kiutendaji  ili kuakisi matakwa ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Hussein Mwinyi  ya kuwapatia  Vijana Ajira Nchini.

Akizungumza na viongozi pamoja na wafanyakazi katika hafla ya ukaribisho  wa Ofisi katika ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Vijana  Migombani, Wilaya ya Mjini.

Amesema ni wajibu wa kila mfanyakazi kufuata muongozo wa ilani ili kufanikisha malengo ya Serikali sambamba na  ushirikiano katika uwajibikaji katika kutekeleza majukumu ya Kazi zao.

Aidha amesema kuwa mwanga wa Matumaini ni mashirikiano ya pamoja ambayo ni  nguzo muhimu ya kufanikisha  malengo  na majukumu Kwa ufanisi mkubwa bila ya kutoka nje ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Nae Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe Hassan Khamis Hafidh  amesema Timu iliyopagwa katika Wizara hiyo ni Timu sahihi  hivyo watahakikisha wanatekeleza azma ya Serikali kuhakikisha Vijana wanafikia ndoto zao .



Amesema Vijana ndio tegemeo la Taifa lolote Duniani na ndio nguvu Kazi ya Taifa tunasikitishwa kwa baadhi ya watu  utayari wao  wa kufanyakazi bado ni mdogo

Nae Katibu Mkuu  Salama Mbarouk Khatib amemshukuru Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Mwinyi  kwa kuwaamini na kuahidi kusimamia vyema  majukumu yao .

 Ameeleza kwamba kutokana na Wizara hivyo ni mpya ni vyema kukamilisha muundo wa Wizara hivyo  kwa haraka ili kuweza kutekeleza majukumu yao Kwa ufanisi.

Mapema Mkurugenzi Utumishi na Uendeshaji wa Wizara ya Habari,Sanaa, Utamaduni na Michezo Rashid Hamdu Makame ameahidi kutoa mashirikiano ya pamoja Kwa Viongozi hao Kwa nia na malengo na kuleta ufanisi .



No comments