Breaking News

KAMATI YA ZAMECO YAWATAKA WAANDISHI WA HABARI KUFANYIA UCHECHEMUZI SHERIA ZA HABARI

                                            

Kamati ya Wataalamu wa Maswala ya Habari Zanzibar (ZAMECO) inaendelea  kuwasititiza wanahabari juu ya kufanya uchechemuzi  wa masuala ya sheria ya habari kwani jambo hilo  bado halijapata muwafaka wake. 

 Hayo yamezungumzwa  8/7/2025  katika mkutano  wa mapitio  ya sheria ya habari uliofanyika katika ofisi za TAMWA  Tunguu Zanzibar ambao uliowajumuisha wajumbe wa Kamati ya ZAMECO,Waandishi wa Habari pamoja na wajumbe wa Baraza la wawakilishi,  kamati hiyo ikasema safari ya kupata sheria rafiki bado haijafika pale tunapopataka licha ya kuwa tumewasilisha jambo hili kwa njia tofauti  kwa viongozi.

Aidha wamesema sheria iliyopo ni ya muda mrefu tangu 1988 na imeshapitiwa na wakati kutokana na kukua kwa teknolojia ya habari ambapo inapelekea vikwazo vikubwa kwa wanahabari na kuwanyima  waananchi taarifa muhimu kutokana na vikwazo vya sheria hiyo.

"Bila ya habari sio rahisi kupata maendeleo  ya kweli  nchi."

Nae Muwakilishi wa Jimbo la Pandani  Professa Omar Fakih Hamad amesema  serikali haijawahi kulikataa suala la wanahabari  kupata  wa sheria hiyo bali suala hilo lipo katika mikakati ya kulipatia ufumbuzi na  kwa mwaka  huu walitarajia  itapatikana lakini halikuwezekana kutokana na bajeti.

Pia alikiri kuwa kuna haja ya kurekebishwa kwa sheria ya habari kwani toka itungwe wakati kipo chama kimoja hadi sasa teknolojia  na mambo mengi yamebadilikana na inapaswa kwendana na mazingira  yaliyopo.

 Amesema wao kama wawakilishi  wataendelea kusimamia sheria hii na wale watakao kuja watawaeleza kwani mara ya mwisho  serilkali iliahidi ipo njiani na mswaada huo utawasalishwa na kupatikana  kwa sheria hio.

" Awamu  5 zijazo Sheria hii ya habari itapatikana katika baraza linazolofata la 11 kwani wawakilishi watalisemezea kupitia mswaada binafsi"

Muwakilishi  wa jimbo la Mfenesini  Mh Machano Othmani Said amewataka waandishi kuendelea kudai sheria yao kwa amani kutokana na kiongozi aliyopo anabusara na an0afahamu umuhimu ya suala hilo  na atatoa suluhisho  kwa jambo hilo.

Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari  Wanawake TAMWA-ZNZ aliwashukuru wawakilishi kwa kuchukua nafasi ya  kulijadili  mswaada  wa sheria ya habari kwa lengo la kupata suluhu ya kusaidia waandishi katika hilo.


No comments